Tetesi Samsung Galaxy S8 Kutokua na Headphone Jack

Tetesi zimesambaa mtandaoni kuhusu samsung galaxy s8 kukosa pini ya headphone maarufu kama headphone jack
Samsung Galaxy s8 Samsung Galaxy s8

Tetesi zimesambaa mtandaoni hivi karibu kuwa kuna uwezekano toleo jipya la simu ya samsung galaxy s8 likaja mapema mwaka 2017 bila sehemu ya kuchomeka pini ya headphone maarufu kama headphone jack.

Badala yake kampuni hiyo inategemea kuweka sehemu ya USB Type-C port ambayo ndio itakuwa sehemu ya kuchaji pamoja na sehemu ya kuchomeka headphone za simu hiyo. Hata hivyo kwa mujibu wa tovuti ya SamMobile, simu hiyo mpya ya Galaxy S 8 inatarajiwa kuja mapema mwaka ujao mwezi February ikiwa na sifa kama kioo cha 2K Super AMOLED  pamoja na sifa zingine nyingi zinazotajwa kwenye tetesi za mitandao mbalimbali.

Kwa mojibu wa tovuti ya thenextweb Samsung imekataa kuzungumia lolote juu ya kukosekana kwa sehemu hiyo maarufu kama heasphone jack. Kwa taarifa kamili tutaendelea kuwapa habari pindi zitakapo tufikia. Unaweza kujiunga nasi kupitia page zetu za Facebook, Instagram, Twitter pamoja na Youtube, pia kwa kupata habari za teknolojia kwa haraka unaweza kudownload App ya Tanzania tech kupitia Play store.

Advertisement

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use