in

Mtandao wa Spotify Wazinduliwa Rasmi Hapa Tanzania

Wasanii na wabunifu wa Tanzania wateza kuweka nyimbo na vipindi mbalimbali

Mtandao wa Spotify Wazinduliwa Rasmi Hapa Tanzania

Mwaka jana 2020, kampuni ya Apple ilizindua rasmi mtandao wa Apple Music Hapa Tanzania, kwa sasa mtandao huo una nyimbo nyingi za wasanii kutoka hapa Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

Sasa baada ya kampuni ya Apple na mtandao wa Apple Music, hivi karibuni kampunia ya Spotify imetangaza kuzindua mtandao wake hapa Tanzania. Mtandao huo unaruhusu wasanii wa hapa nchini Tanzania kuweka nyimbo zao pamoja na vipindi vya mtandao kwa lugha yoyote ikiwa pamoja na Kiswahili.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kwa ujumla mtandao huo utakuwa unapatikana kwa lugha mpya zaidi ya 36 ikiwa pamoja na lugha ya Kiswahili. Watumiaji wote wa hapa nchini Tanzania wataweza kujisajili na mtandao wa Spotify kwa kutengeneza akaunti ya bure na pia kulipia ili kuweza kusikiliza zaidi muziki na vipindi mbalimbali kutoka kwa wasanii na wabunifu mbalimbali.

Mbali ya Tanzania, Spotify inategemewa kuja kwenye nchini nyingine zaidi ya 80 ikiwa pamoja na nchi zote za Afrika mashariki pamoja na Afrika kwa ujumla. Kwa mujibu wa Cnet, list nzima ya nchi ambazo mtandao huo unategemewa kuzinduliwa hivi karibuni ni kama ifuatavyo.

  • Angola
  • Antigua and Barbuda
  • Armenia
  • Azerbaijan
  • Bahamas
  • Bangladesh
  • Barbados
  • Belize
  • Benin
  • Bhutan,
  • Botswana,
  • Brunei
  • Burkina Faso
  • Burundi
  • Cabo Verde
  • Cambodia
  • Cameroon
  • Chad
  • Comoros
  • Côte d’Ivoire
  • Curaçao
  • Djibouti
  • Dominica
  • Equatorial Guinea
  • Eswatini
  • Fiji
  • Gabon
  • Gambia
  • Georgia
  • Ghana
  • Grenada
  • Guinea
  • Guinea-Bissau
  • Guyana
  • Haiti
  • Jamaica
  • Kenya
  • Kiribati
  • Kyrgyzstan
  • Lao People’s Democratic Republic
  • Lesotho
  • Liberia
  • Macau
  • Madagascar
  • Malawi
  • Maldives
  • Mali
  • Marshall Islands
  • Mauritania
  • Mauritius
  • Micronesia
  • Mongolia
  • Mozambique
  • Namibia
  • Nauru
  • Nepal
  • Niger
  • Nigeria
  • Pakistan
  • Palau
  • Papua New Guinea
  • Rwanda
  • Samoa
  • San Marino
  • Sao Tome and Principe
  • Senegal
  • Seychelles
  • Sierra Leone
  • Solomon Islands
  • Sri Lanka
  • St. Kitts and Nevis
  • St. Lucia
  • St. Vincent and the Grenadines
  • Suriname
  • Tanzania
  • Timor-Leste
  • Togo
  • Tonga
  • Trinidad and Tobago
  • Tuvalu
  • Uganda
  • Uzbekistan
  • Vanuatu
  • Zambia and Zimbabwe

Spotify inatarajia kupataikana kwenye sehemu zote ikiwa pamoja na kwenye mtandao yaani website, apps zote za Android na iOS pamoja na apps za kwenye kompyuta. Pia inasemekana kuwa Spotify itaingia kwenye ushirikiano na kampuni mbalimbali kutangaza mtandao huo pamoja na kuweka app hiyo ndani ya vifaa mbalimbali kama smartphone, kompyuta na smartwatch.

Kwa sasa unaweza kupakua app ya Spotify kupitia link hapo chini, kisha jaribu kutengeneza akaunti ili kuanza kusikiliza kwa urahisi nyimbo za wasanii mbalimbali kutoka Afrika na dunia.

  • Android App

Download App Hapa

  • iOS App

Download App Hapa

Mtandao wa Spotify Wazinduliwa Rasmi Hapa Tanzania

Pia unaweza kutumia mtandao wa Spotify kwa lugha ya Kiswahili kupitia website yake kwa kutembelea mtandao huo kupitia link hapo chini.

Tembelea Tovuti Hapa

Mtandao wa Spotify Wazinduliwa Rasmi Hapa Tanzania
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.