in

Ugumu na Ubora wa Simu Yenye Kamera Chini ya Kioo

ZTE Axon 20 5G ni simu ya kwanza yenye kamera ya mbele chini ya kioo

Ugumu na Ubora wa Simu Yenye Kamera Chini ya Kioo

Kama wewe ni mfuatiliaji wa Tanzania tech hasa kipengelea cha simu mpya basi ni wazi kuwa unafahamu kuhusu simu mpya ya ZTE Axon 20 5G, simu hii imeshika vichwa vya habari sana siku za karibuni kutokana na kuwa simu ya kwanza kuwa na kamera ya mbele chini ya kioo.

Kifupi ni kwamba, ZTE Axon 20 5G inakuja na kioo kizima yani full display ambapo hakuna kingo kubwa kama simu nyingine, na pia haina hata sehemu ya spika ya kusikilizia simu kwani nayo inapatikana chini ya kioo.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Ugumu na Ubora wa Simu Yenye Kamera Chini ya Kioo

Kama unavyoweza kuona simu hii inakuja na kioo kitupu na pia inakuja na spika iliyopo chini ya kioo pamoja na sehemu ya ulinzi ya fingerprint nayo inapatikana chini ya kioo. Lakini je vipi kuhusu ubora na ugumu wa simu hii mpya. Kufahamu hayo unaweza kuangalia video hapo chini.

Tayari ZTE Axon 20 5G inapatikana kote duniani ikiwa pamoja na Uingereza, Korea Kusini, Urusi, Thailand, Malaysia, Ufilipino, UAE, Saudi Arabia na Afrika Kusini. Kama tayari simu hii inapatikana Afrika kusini basi siku sio nyingi utaweza kununua simu hii hapa nchini Tanzania.

Kumbuka simu hizi zinapatikana kwa matoleo mawili ZTE Axon 20 5G na ZTE Axon 20 4G, unaweza kuangalia tofauti ya simu hizi hapa.

Ugumu na Ubora wa Simu Yenye Kamera Chini ya Kioo
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Infinix na JBL Waungana Tena Na Sasa Ni Infinix Note 40

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.