in

Facebook Yanunua Mtandao wa Giphy kwa TZS Bilioni 926

Kampuni ya facebook yazidi kuongeza ukubwa wa mtandao wake zaidi

Facebook Yanunua Mtandao wa Giphy kwa TZS Bilioni 926

Kampuni ya Facebook hivi karibuni imetangaza kununua mtandao wa Giphy kwa dollar za marekani milioni $400, sawa na takribani zaidi ya bilioni 900 za kitanzania. Giphy ni mtandao wa kijamii ambao unajulikana kwa kuwa na idadi kubwa ya watumiaji wanaoshiriki picha au video fupi ambazo hazina sauti maarufu kama GIF.

Facebook Yanunua Mtandao wa Giphy kwa TZS Bilioni 926

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kwa mujibu wa Facebook, mtandao wa Giphy utaendelea kufanya kazi kama kawaidia bila mabadiliko yoyote kwa sasa, lakini facebook inategemea kuongeza watumiaji kwenye mtandao huo kwa kuunganisha mtandao huo moja kwa moja na mtandao wa instagram ambao tayari unayo sehemu ya kushiriki picha hizo zinazotembeea maarufu kama GIF.

Facebook Yanunua Mtandao wa Giphy kwa TZS Bilioni 926

“Watumiaji wanaweza kuendelea kuweka picha zao zinazo tembea kupitia mtandao wa Giphy bila kuwa na mabadiliko yoyote hadi hapo kampuni hiyo itakapo tangaza kufanya mabadiliko”, ilisema sehemu ya taarifa kutoka mtandao wa Facebook.

Hata hivyo inasemekana kuwa inawezekana kuwa facebook imetoa pesa nyingi zaidi kutokana na kuwa kiwango kilichotajwa hapo juu ni makadirio na sio kiwango ambacho facebook yenyewe imethibitisha. Kwa mujibu wa mtandao wa tovuti ya Reuters, inasemekana kuwa facebook ilikataa kutaja kiwango cha pesa ambacho ili lipa kununua mtandao huo.

Kama wewe ni mmoja wa watu ambao unataka kujua kuhusu mtandao huo wa Giphy, unaweza kupakua app yake kupitia Play Store au unaweza kutembelea tovuti ya Giphy.com ili kutengeneza akaunti.

Facebook Yanunua Mtandao wa Giphy kwa TZS Bilioni 926
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

2 Comments