in

Aga Khan Yaja na CoronaCheck App Maalum kwa Watanzania

Sasa utaweza kujitathmini ukiwa nyumbani kwa kutumia CoronaCheck App

Aga Khan Yaja na CoronaCheck App Maalum kwa Watanzania

Kwa mujibu wa tovuti ya The Citizen, Hivi sasa watanzania wanaweza kutathmini kwa urahisi na kwa usalama dalili za Covid-19 kwa kutumia njia mpya wakiwa nyumbani, shukrani kwa mpango mpya wa Huduma ya Afya ya Aga Khan na Chuo Kikuu cha Aga Khan (AKU).

Kwa mujibu wa tovuti hiyo, Asasi hizo mbili zimezindua programu mpya ya Android na iPhone ambayo inaruhusu watu kutathmini kwa urahisi dalili za Covid-19 wakiwa nyumbani na kwa hivyo, kujua hatua zifuatazo baada ya kujua afya yao. App hiyo iliyopewa jina la CoronaCheck, inaweza kupakuliwa kwenye soko la Play Store na App Store bila Malipo yoyote.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Aga Khan Yaja na CoronaCheck App Maalum kwa Watanzania

Kupitia app hiyo ambayo ipo kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza, utaweza kujibu maswali mbalimbali kuhusu afya yako ikiwa pamoja na kueleza kama unajisikia dalili za tofauti katika mwili wako. Pia kupitia app hiyo utaweza kupata vidokezo vya muhimu kuhusu virusi vya corona, pamoja na kupata namba za dharura za kutoa taarifa kuhusu COVID-19.

Programu hiyo ni ya kwanza kwa hapa Tanzania, lakini sio programu ya kwanza ambayo inatoa nafasi ya kuelimisha kuhusu virusi vya corona. Wiki chache zilizopita, pia serikali ya Australia ilizindua app maalum ya kusaidia kutambua kwa urahisi walio ambukizwa virusi vya corona iliyokuwa inaitwa CovidSafe.

Kwa sasa kama upo hapa Tanzania unaweza kupata app hii mpya ya Corona Check kupitia masoko ya Play Store au App Store au kama link hizo hazifanyi kazi unaweza kubofya link hapo chini.

CoronaCheck – Android

CoronaCheck
Price: Free

CoronaCheck – iOS

‎Corona-Check
Price: Free
Aga Khan Yaja na CoronaCheck App Maalum kwa Watanzania
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Apps Muhimu kwaajili ya Mwezi wa Ramadhani (2024)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.