in

Njia Mpya za Kutumia Browser ya Google Chrome (Android)

Hivi ndivyo unavyoweza kupata sehemu ya Dark Mode kwenye Google Chrome

Njia Mpya za Kutumia Browser ya Google Chrome (Android)10:37

Kama wewe ni mtumiaji wa simu ya Android basi ni lazima utakuwa unatumia browser ya Google Chrome, hii ni kwa sababu mara nyingi mfumo wa Android unakuja na browser ya Google Chrome ndani ya simu zote zenye mfumo wa Android. Hii ni kwa sababu mfumo wa Android unakuja na vigezo na masharti ya kuweka app za Google kwenye kila simu inayotumia mfumo huo.

Anyway, kama unatumia browser hiyo basi leo nimekuandalia maujanja mbalimbali ambayo unaweza kufuata ili kubadilisha muonekano wa kivinjari hicho ikiwa pamoja na kufanya kivinjari kuweza kufanyakazi kwa haraka zaidi. Basi bila kupoteza muda twende tukajifunze maujanja haya.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kwa kufuata maujanja yote hayo basi najua utakuwa umeweza kufanya kivinjari chako cha Chrome kuwa na muonekano mpya pamoja na kufanya kazi kwa haraka zaidi. Maelezo zaidi unaweza kupata hapo chini.

  1. Kama unataka kufanya app ya Chrome iweze kudownload kwa haraka utaandika – enable parallel download
  2. Kama unataka kubadilisha mahali vitu unavyo download vinapo hifadhiwa andika – enable download location change
  3. Kama unataka kubadilisha sehemu za Home Screen pamoja na sehemu ya kusearch viamie kwa chini basi andika – Home Duet
  4. Kama unataka kuongeza Speed ya kufungua tovuti mbalimbali basi andika – QUIC Protocol
  5. Kama unataka kuwasha sehemu ya Dark Mode basi unatakiwa kudownload app ya Chrome Canary kisha andika chrome://flags kwenye browser hiyo na kisha andika – Dark Mode

Na hayo ndio maujanja niliyo kuandalia kwa siku ya leo, kama kuna mahali umekwama unaweza kuuliza kupitia sehemu ya maoni hapo chini pia kwa maujanja zaidi hakikisha unapitia hapa kujifunza jinsi ya kutumia app za kulipia za android bure kabisa.

Njia Mpya za Kutumia Browser ya Google Chrome (Android)
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Jinsi ya Kujua Mafile Yanayochukua Nafasi Kubwa (Kompyuta)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

2 Comments