in

Ubunifu wa Kitanzania Teknolojia ya Kuzuia Wizi wa Magari

Inawezekana hii ndio dawa ya wizi wa magari Tanzania..?

Ubunifu wa Kitanzania Teknolojia ya Kuzuia Wizi wa Magari

Habari siku ya leo kutoka Tanzania, Wabunifu wa teknolojia kutoka hapa nchini wamekuja na mfumo mpya ambao unaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa kuzuia wizi wa magari hasa hapa nchini Tanzania.

Wakihojiwa kupitia millardayo, wabunifu hao ambao ni wakazi wa jijini Dar es salaam wamekuja na teknolojia hiyo ambayo itamuwezesha mtu kuzima na kuwasha gari lake popote pale alipo, ikiwa pamoja na kupata data za mahali gari lake lilipo kupitia GPS pamoja na mambo mengine mengi.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Mfumo huo ambao unafungwa kwenye gari, kwa sasa tayari unatumika kwenye magari zaidi ya 200 hapa nchini Tanzania huku magari hayo yote yakiwa salama kutokana na kusaidiwa na mfumo huo ulio buniwa na vijana wa kitanzania. Kujua zaidi kuhusu mfumo huo angalia video hapo chini.

Je nini maoni yako kuhusu ubunifu huu, unadhani unaweza kusaidia kupunguza uwizi wa magari hasa hapa kwetu Tanzania..? Tuambie kupitia sehemu ya maoni hapo chini.

Ubunifu wa Kitanzania Teknolojia ya Kuzuia Wizi wa Magari
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

2 Comments