2009 Vs 2019 Mambo Mbalimbali ya Teknolojia #10Yearschallenge

Haya hapa ndio mabadiliko makubwa ya teknolojia kutoka 2009 hadi sasa 2019
2009 Vs 2019 Mambo Mbalimbali ya Teknolojia #10Yearschallenge 2009 Vs 2019 Mambo Mbalimbali ya Teknolojia #10Yearschallenge

Ukweli ni kwamba teknolojia imekuwa sana kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita hadi sasa, hapa nazungumzia kutokea mwaka 2009 hadi sasa mwaka 2019. Hi, karibu Tanzania Tech na kwa kuanza najua tayari umesha shirikia au pengine umesha fanikiwa kuona picha mbalimbali zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikiwa na hashtag ya #10Yearschallenge.

Sasa baada ya kuona challenge hii kwa watu wengi, hatimaye Tanzania tech tumeamua kuangalia #10Yearschallenge ya mambo mbalimbali ya kiteknolojia. I Hope utaenda ku-enjoy pamoja na kujifunza jinsi teknolojia inavyozidi kukuwa kila siku.

Mauzo ya Simu 2009 Vs 2019

Japo kuwa utaona kama ni juzi tu ila 2009 teknolojia ilikuwa bado inajikongoja, kipindi hicho kwenye upande wa mauzo ya Simu Nokia 5230 ndio ilikuwa simu inayoongoza kwa mauzo kwa kuwa na mauzo ya nakala zaidi ya milioni 159 kwa mwaka mzima.

Advertisement

Nokia 5230
Nokia 5230

Mwaka 2019 kutokea 2018 mauzo ya simu yamekuwa tofauti kidgo na sasa kwani kwa kipindi hicho kampuni ya Nokia haikuwa hata kwenye Top 3 ya mauzo ya simu kwa mwaka 2018 – 2019. Mwaka jana 2018 simu iliyokuwa inaongoza kwa mauzo ni Samsung Galaxy Note 9 kwa kuuza nakala zaidi ya milioni 30 kwa mwaka mzima tokea simu hiyo ilipo zinduliwa.

Galaxy Note 9 #10Yearschallange
Galaxy Note 9 #10Yearschallange

Simu ya Bei Ghali 2009 Vs 2019

Kwa kuwa teknolojia inaendelea kukuwa kila siku, hata mwaka 2009 ulikuwa ni mwaka wa kupiga hatua kwa kampuni mbalimbali za kiteknolojia. Mwaka huu ndipo kampuni ya Apple ilizindua simu mpya ya iPhone 3GS, Simu hii ilikuwa ni moja kati ya simu nzuri sana na pia ndio iliyochukua chati ya kuwa simu ya bei ghali kwa mwaka huo. Sasa hapa siongelei iPhone 3GS ya kawaida bali nazungumzia iPhone 3GS SUPREME ambayo ilikuwa imetengenezwa kwa Gold na Almasi.

iPhone-3GS-SUPREME
iPhone 3GS SUPREME

Simu hii imetengenezwa kwa Pure Gold na kama unavyoweza kuona ilikuwa na mkanda wa almasi mbela, na nyuma logo ya Apple pia ilikuwa imetengenezwa kwa almasi na kwenye kitufe cha home kulikuwa na jiwe la almasi ambalo ni hadimu sana. Kwa ujumla simu hii ilikuwa na samani ya dollar za marekani milioni $3.15 sawa na takribani Tsh bilioni 7.26.

Mwaka 2018 kuja 2019, bado kuna simu nyingi ambazo ni za bei ghali lakini zote haziwezi kushindana na simu hii ya iPhone 4. Simu hii sio iPhone ya kawaida bali hii ni iPhone 4 Diamond Rose ambayo imetengenezwa kwa almasi hadimu sana na kufanya thamani ya simu hii kupanda na kufikia dollar za marekani milioni $8 ambayo ni sawa na takribani shilingi za Tanzania Tsh Bilioni 18.4.

iphone-4-diamond-rose

Samsung Galaxy 2009 Vs 2019

Kama nilivyo sema mwaka 2009 ulikuwa ni mwaka wa kihistoria kwa makampuni mengi sana ya kiteknolojia, historia hiyo pia ipo kwa kampuni ya Samsung kwani mwaka 2009 kampuni hiyo ilitoa mfululizo wa kwanza wa simu za Samsung Galaxy. Simu hiyo ya kwanza ya Samsung Galaxy iliyopewa jina la Samsung GT-I7500 au Samsung Galaxy (original) ni moja ya simu ambazo pia zilikuwa na teknolojia ya kisasa na muundo mzuri kwa kipindi hicho.

Samsung Galaxy (original)

Kwa mwaka huu 2019 Simu za samsung galaxy zimebadilika sana na karibia kila mwezi simu mpya za Samsung Galaxy zimekuwa zikitoka zikiwa na teknolojia ya kisasa kabisa. Kwa mwaka huu 2019 toleo jipya la Samsung Galaxy F ndio toleo la simu za Samsung Galaxy ambalo linategemewa kuwa toleo la kisasa na lenye muundo mzuri, huku ikifatiwa na Samsung Galaxy S10 ambayo pia inategemewa kuwa simu ya kisasa na yenye muonekano mzuri.

Samsung Galaxy F
Samsung Galaxy F

Gari la Mwaka 2009 Vs 2019

Tuzo za gari la mwaka au World Car Awards (WCOTY) zilianzishwa mwaka 2003 na ili kusudi gari liweze kushiriki linatakiwa liwe maarufu angalau kwenye nchi 5 au kwenye mabara mawili na iwe ni kabla ya january 1 kabla ya kuanza kwa tuzo hizo.

Mwaka 2009 gari lililo shilkilia chati ya gari la mwaka huo ilikuwa ni Volkswagen Golf Mk6, Gari hili kwa mwaka huu ni gari la kawaida sana yani ni sawa na kusema Vits wala sio IST.

Volkswagen Golf Mk6
Volkswagen Golf Mk6

Kwa mwaka 2018 kuelekea 2019 mambo ni tofauti sana tena ukizingatia kwa sasa kuna magari mengi sana yanayotumia umeme. Mwaka 2018 gari ambalo limeshikilia chati ya kuwa gari bora la mwaka ni Volvo XC60.

Volvo XC60
Volvo XC60

Kama unataka kujua zaidi kuhusu vigezo na masharti vilivyo tumika unaweza kusoma zaidi kuhusu tuzo hizi kupitia mtandao wa Wikipedia Hapa.

Apple 2009 Vs 2019

Kama umesoma makala nzima kuanzia mwanzo basi lazima utakuwa umeona mwaka 2009 ulikuwa na umuhimu gani kwa kampuni ya Apple. Ila kama ujasoma basi labda ni kwambie kuwa mwaka 2009 ni mwaka muhimu kwa Apple kwani kampuni hiyo ndipo ilipotoa simu mpya ya iPhone 3GS.

iPhone 3GS iOS
iPhone 3GS iOS

Fast Forward mwaka 2018 kuelekea 2019, Apple ni kampuni ya tofauti sana na mwaka 2018 kampuni hiyo imetangazwa kuwa kampuni yenye thamani ya Trilioni 1 za marekani. Lakini pamoja na hayo bado kampuni hii iko kwenye chati ya simu bora za mwaka 2018 kwa kuwa na simu zinazo tumiwa zaidi na watu wengi.

iPhone XS na XS Max
iPhone XS na XS Max

Nadhani mpaka hapo unaona jinsi gani teknolojia ilivyoweza kubadilika kwa kasi sana, mambo yapo mengi sana ambayo pengine tukiandika hapa tutachukua zaidi ya kurasa mbili na najua wengi wetu hatupendi kusoma maneno mengi.

Anyway kwa leo hii ndo #10Yearschallange ambayo tumeona kushiriki na nyie, mpaka siku nyingine guys endelea kupitia tovuti ya Tanzania Tech kila siku kifunza mambo mengi zaidi kuhusu teknolojia.

1 comments
  1. Habari ndugu!
    Kuna simu moja nimeichukua China, simu aina ya Huawei Nova 3e, sasa nikitaka kujisajiri kwenye Huawei ID, inanionyesha imeshasajiriwa kwa namba za China.
    Sasa nitawezaje kuisajiri kwa ID ya Tanzania nahitaji msaada wenu ndugu zangu
    Wenu katika habari za Teknolojia
    Ndg Erick Gulayi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use