in

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp

Sasa unaweza kutumia stickers rasmi kupitia app ya WhatsApp

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp

Baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu hapa Tanzania hatimaye hivi leo sehemu mpya ya Stikers ndani ya WhatsApp imewezeshwa rasmi, hivyo basi kuanzia leo utaweza kutuma stickers moja kwa moja kupitia App ya WhatsApp.

Mbali na kuwa na uwezo wa kutuma stika pia kupia maujanja mbalimbali sasa utakuwa na uwezo wa kubadilisha baadhi ya picha na kuwa sticker, lakini kabla ya kuangalia hilo labda tungalie kwanza jinsi ya kupata sehemu hii mpya sticker kupitia kwenye app yako ya Android na iOS.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Sasa ili kupata sehemu hii, Sticker unachotakiwa kufanya ni kubofya sehemu ya Emoji kisha kwa chini utaona sehemu mpya ambayo itakuwa na kidoti chekundu kama ndio mara yako ya kwanza kufungua sehemu hiyo, bofya hapo na utona sticker mbalimbali zimefunguka.

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp

Chagua sehemu ya emoji kama inavyo onekana kwenye picha hapo juu kisha chagua sehemu ya mwisho kabisa chini upande wa kulia karibia na GIF, kama inavyo onekana kwenye picha hapo chini.

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp

Kwa upande wa iOS ni tofauti kidogo na rahisi kuliko Android, kupitia app ya WhatsApp ya iOS fungua app hiyo kisha utaona sehemu ya Sticker pembeni ya chumba cha kuandikia ujumbe, bofya hapo na utapelekwa moja kwa moja kwenye mkusanyiko wa stika mbalimbali.

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp

Jinsi ya kutengeneza Sticker zako Mwenyewe

Sasa kama tayari umeshaweza kuona sehemu hiyo mpya basi unaweza kuendelea kuitumia na zaidi ni kuwa unaweza kupakua app mbalimbali za sticker na utaweza kuzitumia moja kwa moja kwenye app ya WhatsApp. Lakini mbali na hayo pia unaweza kutengeneza sticker kutokana na picha zako mwenyewe.

Njia hii ni rahisi sana na unaweza kufanya sasa hivi. Unachotakiwa kufanya ni kudownload App ya Sticker Studio kisha anza kwa kuweka picha yako kisha baada ya hapo kata picha zako kwa kuzungushia duara sehemu unazotaka zibaki, kisha save alafu bofya kutufe cha jumlisha.. Done!! hapo WhatsApp itaweza kufunguka na kukwambia sticker mpya imeongezwa. Unaweza kudownload app hiyo kupitia link hapo chini.

Kuanzia Leo Tuma Stickers Kwa Kutumia WhatsApp
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Apps Muhimu kwaajili ya Mwezi wa Ramadhani (2024)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

4 Comments