Muonekano wa iPhone Xs Wavuja Kabla ya Uzinduzi

Muonekano wa simu mpya ya iPhone Xs wavuja kabla ya kuzinduliwa
Muonekano wa iphone Xs Muonekano wa iphone Xs

Kampuni ya Apple ni moja kati ya kampuni zenye msimamo mkali sana kuhusu uvujishaji wa bidhaa zake kabla ya kuzinduliwa rasmi, mwaka jana kampuni ya Apple ilimfukuza kazi mhandisi wake baada ya mtoto wa mhandisi huyo kuonyesha muonekano wa iPhone X kabla ya simu hiyo kuzinduliwa rasmi.

Lakini pamoja na Apple kuwa na msimamo mkali kuhusu uvujishaji wa aina hiyo bado ni ngumu sana kuweza kuzuia uvujishaji kwa asilimia 100 ukizingatia simu hizi hupitia kwenye mikono ya watengenezaji wengi pamoja na makampuni mbalimbali kabla ya kuingia sokoni.

Sasa ikiwa yamebaki masaa kadhaa hadi kuzinduliwa rasmi kwa simu mpya za iPhone Xs, iPhone Xs Plus pamoja na iPhone Xc, tayari kumesha sambaa picha zenye muonekano wa simu mpya inayo tarajiwa ya iPhone Xs. Simu hiyo kwa muundo haitofautiani kabisa na simu ya mwaka jana ya iPhone X ila tu ukubwa wa simu hii ya sasa umeongezwa na kufikia inch 6.8 kutoka ukubwa wa simu ya mwaka jana ya iPhone X ambayo ilikuwa na inch 5.8.

Advertisement

Kwa sasa bado hakuna tetesi yoyote inayoelezea kuhusu sifa za simu hii ila kwa sababu yamebaki masaa machache, basi tukutane kwenye uzinduzi wa simu hizi mpya ambao utonyeshwa mubashara kabisa kupitia hapa Tanzania Tech siku ya leo kuanzia majira ya saa mbili kamili za usiku.

Kama wewe ni mpenzi wa bidhaa za Apple nakusihi usikose kutizama uzinduzi huo mubashara kabisa kupitia hapa Tanzania Tech.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use