Muonekano wa BlackBerry Key2 Wavuja Kabla ya Uzinduzi

Huu ndio muonekano wa simu mpya ya BlackBerry Key2
Muonekano wa blackberry-key2 Muonekano wa blackberry-key2

Hivi karibuni, Blackberry ilitangaza kuwa inajiandaa na uzinduzi wa simu yake mpya ya BlackBerry Key2, Simu hii ni mwendelezo wa toleo la Blackberry KeyOne ambayo ilizinduliwa mwaka jana.

Habari mpya hivi karibuni ni kuhusu muonekano wa simu hiyo ya BlackBerry Key2 muonekano ambao umevujishwa mapema kabla ya kuzinduliwa rasmi kwa simu hiyo. Muonekano huo umevujishwa na mvujishaji maarufu wa mambo ya teknolojia kupitia mtandao wa Twitter anae itwa Evan Blass.

Kwa kuangalia muonekano wa simu hiyo ya BlackBerry Key2 hapo juu, ni wazi simu hiyo haina tofauti sana na toleo lilio pita la simu ya BlackBerry KeyOne. Tofauti kubwa iliyopo kwenye toleo la sasa ni uwepo wa kamera mbili kwa nyuma na kitufe kipya kinacho onekana upande wa kulia chini kwenye keyboard ya simu hiyo.

Advertisement

Mbali na hayo bado hakuna mabadiliko mengine mengi kwa upande wa muonekano wa simu hii, labda tusubiri mpaka tarehe 7 ya mwezi huu ambapo BlackBerry ndio itaenda kuzindua rasmi simu hiyo ya BlackBerry Key2 na Tutakujuza zaidi kuhusu sifa kamili za ndani za simu hiyo bila kusahau na makadirio ya bei yake kwa hapa Tanzania.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use