Hatimaye Chuo cha Tanzania cha DIT Kuanza Kuunda Roboti

Licha ya DIT, vyuo vingine ni pamoja na vyuo vya kenya, Ghana na Afrika Kusini
DIT kutengeneza Roboti DIT kutengeneza Roboti
<a href="http://www.parcrobotics.org/" rel="nofollow" target="_blank"><span style="font-size: x-small;">Picha na Parcrobotics.org</span></a>

Hivi karibuni ripoti kutoka gazeti la mwananchi zinasema, Siemens ni miongoni mwa kampuni zin-azongoza kwenye uendelezaji wa taaluma ya artificial intelligence inayohamasisha ubunifu na uundaji wa roboti. Baada ya uzoefu wa miaka mingi, kam-puni hiyo imeamua kuongeza ushawishi wake Afrika kwa kuvijengea uwezo baadhi ya vyuo vikuu ili kuihamishia teknolojia hiyo barani humu.

Katika mpango huo, Chuo cha Teknolojia Dar es Salam (DIT) kinakuwa miongoni mwa vyuo 13 vya Afrika vilivyopewa mitambo ya kuunda roboti na kampuni ya Siemens. Mkuu wa kitengo cha uhusiano wa viwanda na taasisi wa DIT ambaye ni mratibu wa ushirikiano kati ya Siemens na chuo hicho, Dk John Msumba anasema uhusiano kati yao ulianza mwaka 2016.

Anasema mwaka huo, kampuni hiyo ilianzisha programu ya kutafuta mabalozi kwenye mataifa mbalimbali Afrika na taasisi hiyo ya elimu ya juu ikakidhi vigezo. Katika ushirikiano huo, Dk Msumba anasema: “Wanayo lab (maabara) itakayotumika kufundishia wanafunzi pamoja na wateja wa bidhaa zao. Ushirikiano huu unatoa fursa ya kuwa na wataalamu wa kusimamia viwanda vinavyohitaji teknolojia ya kisasa hata kuvifufua vilivyokufa.”

Advertisement

Anasema kwenye hatua za awali msisitizo umeelekezwa kuandaa wataalamu wenye viwango vinavyokubalika kimataifa jambo litakalozishawishi kampuni za ndani au nje kuanzisha uzalishaji. “Wanafunzi wetu wameshatengeneza mitambo mingi lakini haijaendelezwa kwa kuwa DIT ni taasisi ya elimu si kampuni ya uzalishaji. Wakitokea wawekezaji, mambo mengi yatabadilika,” anasema.

Dk Msumba anasema Siemens wameshaleta Programmable Logic Controllers (PLC); mitambo inayotumika kuingiza maelekezo ya majukumu yatakayotekelezwa na roboti husika na kinachosubiriwa ni kompyuta maalumu zitakazofanikisha mawasiliano kati ya wataalamu na mashine husika. Mwezi uliopita, kampuni hiyo ilitangaza kutenga Dola 400,000 za Marekani (zaidi ya Sh896 milioni) kwa ajili ya kusambaza vifaa hivyo kwenye vyuo vikuu inavyoshirikiana navyo.

Ofisa mtendaji mkuu wa Siemens; kusini na mashariki mwa Afrika, Sabine Dall’Omo anasema tofauti ya maendeleo kati ya Afrika na mabara mengine inaweza kuondolewa kwa matumizi ya teknolojia hasa iliyotengenezwa sehemu husika kukabili changamoto zilizopo.

“Teknolojia ni muhimu Afrika lakini manufaa yake yataonekana endapo kutakuwa na mafunzo sahihi yanayotolewa kwa vijana na vifaa vya uhakika kufanikisha lengo lililokusudiwa,” anasema Dall’Omo.

Hata hivyo Vyuo vingine vitakavyo nufaika na mpango huo ni vya mataifa ya Tanzania, Ghana, Kenya na Afrika Kusini. Licha ya DIT, vingine vilivyo jumuishwa ni Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Kwame Nkrumah (Ghana) na Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Dedan Kimathi (Kenya) pamoja na vyuo vikuu tisa vya Afrika Kusini.

Ripoti Kutoka Gazeti la Mwananchi

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use