in

Galaxy S7, A3, A5 na A7 Kupata Toleo la Android 8 Mwezi May

Kama unatumia simu hizo tegemea toleo la Android Oreo Kuanzia mwezi May

Samsung-Galaxy-S7-Edge

Hivi karibuni watumiaji wengi sana wanaotumia simu za Android wamekuwa wakitamani kupata toleo jipya la Android 8 au Android Oreo kwenye simu zao za Android. Lakini kwa watumiaji wa simu za Samsung ni wazi kuwa kampuni ya Samsung imekuwa taratibu sana kutoa matoleo mapya ya Android kwenye simu mbalimbali za Android na kufanya watumiaji kusubiri kwa muda mrefu sana.

Japokuwa hivi karibuni tulipata list ya simu za Samsung ambazo zinaweza kupata kupata toleo la Android Oreo, lakini vilevile kwenye list hiyo ni baadhi ya simu tu ambazo tayari zimepata toleo hilo la Android Oreo. Lakini sasa kwa mujibu wa tovuti ya GSM Arena, kama wewe ni mmiliki wa simu za Samsung Galaxy S7, Galaxy A3 (2017), Galaxy A5 (2017), pamoja na Galaxy A7 (2017) basi tegemea kupata toleo jipya la Android Oreo au Android 8.0 siku za karibuni.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Ripoti hizo pia zinabainisha tarehe halisi ya kutoka kwa toleo hilo ni kuanza tarehe 18 May na simu za Galaxy S7 na S7 Edge ndizo zitakuwa za kwanza kupata toleo hilo ikifuatiwa na Simu nyingine kwenye list hii za A3, A5, alafu A7 zote zikiwa ni simu za mwaka 2017.

Hata hivyo inawezekana kuwa toleo hilo likachelewa kidogo kwa Tanzania, hivyo kama wewe ni mtumiaji wa simu hizo na upo Tanzania au Afrika mashariki kwa ujumla tegemea toleo hilo ndani ya mwezi wa tano mwaka huu 2018 au mwanzoni mwa mwezi wa sita mwaka huu 2018.

Galaxy S7, A3, A5 na A7 Kupata Toleo la Android 8 Mwezi May
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Infinix na JBL Waungana Tena Na Sasa Ni Infinix Note 40

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

2 Comments