in

Tigo Yaungana na Mastercard Kuleta Huduma ya Masterpass QR

Tigo Tanzania Kuanza kupokea husuma za Masterpass QR

Tigo Tanzania Masterpass QR

Kampuni inayotoa huduma za simu ya Tigo Tanzania hivi karibuni imeungana rasmi na kampuni ya huduma za kifedha ya MasterCard ili kuleta huduma ya Masterpass QR kwa watumiaji wa huduma za kifedha za Tigo Pesa.

Ripoti kutoka tovuti ya Business Chief zinasema, MasterCard imetangaza hayo kupitia mkutano wa MWC 2018 au Mobile World Congress unaofanyika huko nchini Barcelona. MasterCard kupitia kwa msemaji wake imesema kuwa imeamua kuungana na Tigo Tanzania kwa sababu huduma ya Tigo Pesa ni moja kati ya huduma inayo tegemewa sana Hapa Tanzania huku ikiwa na watumiaji zaidi ya milioni 7 ambao watenda kufurahia huduma hiyo.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Masterpass QR ni huduma inayo mruhusu mteja kuweza kulipia bidhaa mbalimbali kwa urahisi kwa kutumia simu ya mkononi kwa kuscan QR code maalum kwa kutumia kamera ya simu ya mkononi na hii uleta urahisi kati ya muuzaji wa bidhaa pamoja na mteja kwa kurahisha njia ya malipo.

Hata hivyo huduma hiyo inategemewa kuwezeshwa kwenye Programu ya Tigo Pesa App ambapo wateja wa Tigo wataweza kulipia bidhaa kwa urahisi kupitia App hiyo. Huduma hii inategemewa kuwezeshwa baadae katikati ya nusu ya mwaka huu 2018. Kujua zaidi kuhusu Masterpass QR tembelea ukurasa huu.

Tigo Yaungana na Mastercard Kuleta Huduma ya Masterpass QR
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.