in

Snapchat Kuja na Sehemu ya “Mention” Kwenye Stories

Sasa Snapchat imeamua chukua sehemu kutoka mtandao wa Instagram

Snapchat Kuja na Sehemu ya "Mention" Kwenye Stories

Tumesha zoea kuwa mara nyingi instagram ndio inayochukua baadhi ya sehemu za mtandao wa Snapchat na kuweka kwenye mtandao wake, lakini hivi karibuni Snapchat imeamua kuanza kuchukua sehemu za Instagram kuweka kwenye mtandao wake hasa sehemu ya Stories.

Hivi leo imeripotiwa kuwa, Snapchat inafanyia majaribio ya sehemu mpya ya Mention kwenye sehemu ya Stories kama ilivyo kwenye mtandao wa Instagram. Sehemu hii inafanya kazi sawa na sehemu ya Stories kwenye Instagram. Yaani unaweka alama ya @ na kuweka username ya mtu kwenye picha yako au kwenye sehemu ya maelezo ya picha yako na utakuwa umeweza kumtag mtu kwenye sehemu ya Stories kama ilivyo kwenye instagram.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Utofauti ulipo kwenye sehemu ya mention ya kwenye Snapchat stories ni kuwa, sehemu hii haionyeshi list ya majina pale unapo anza kuandika alama ya “@” kama ilivyo kwenye Instagram, bali itakubidi ukumbuke username kamili ya mtu unaye taka kumtag kwenye sehemu ya Stories kupitia App za Snapchat.

Msemaji wa mtandao wa Snapchat imeambia tovuti ya Tech Crunch kuwa, kwa sasa inafanya majaribio ya sehemu hiyo na bado sehemu hiyo haijaweza kuwezeshwa kwa kila mtumiaji wa mtandao huo. Endelea kutembelea Tanzania Tech kupata Taarifa zaidi kuhusu sehemu hii.

Snapchat Kuja na Sehemu ya "Mention" Kwenye Stories
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Hizi Hapa Browser Bora Zenye Mfumo wa Akili Bandia (AI)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.