Hatimaye Mazungumzo Baina ya Serikali na Airtel Yaanza

Baada ya sakata la umiliki wa kampuni hiyo sasa mazungumzo yaanza
Hatimaye Mazungumzo Baina ya Serikali na Airtel Yaanza Hatimaye Mazungumzo Baina ya Serikali na Airtel Yaanza

Mazungumzo baina ya kampuni ya simu ya Airtel Tanzania pamoja na serikali Tanzania yameanza rasmi huku Mazungumzo hayo yakiwa yanalenga kufikia makubaliano yatakayokuwa na tija kwa pande zote mbili na kuimarisha sekta ya mawasiliano Tanzania.

Hata hivyo mazungumzo hayo yanakuja baada ya kuibuka utata hapo Desemba mwaka jana kuhusu mmiliki halali wa Airtel Tanzania, Serikali ikisema ndiyo mmiliki halali kwa sababu ubinafsishwaji wa kampuni hiyo haukufuata utaratibu madai ambayo yalikanushwa na kampuni ya Bharti Airtel.

Kwa mujibu wa gazeti la mwananchi, Mazungumzo hayo yanafanyika jijini Dar es Salaam, huku serikali ikiwakilishwa na mwenyekiti wa kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, Upande wa Bharti Airtel unawakilishwa na mwanasheria mkuu wake anae julikana kwa jina la Mukesh Bhavnani.

Advertisement

Taarifa hiyo imetolewa leo Machi 12, 2018 na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu, huku ikisisitiza kuwa mazungumzo hayo yana lengo la kufikia makubaliano yatakayokuwa na tija kwa pande zote mbili na kuimarisha sekta ya mawasiliano Tanzania.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use