Apple Kuja na Laptop ya MacBook Air ya Bei Nafuu Zaidi

Apple kutegemewa kuja na laptop ya bei rahisi zaidi
Macbook Air Macbook Air

Ripoti kutoka kwa mwanaripoti wakuaminika Ming-Chi Kuo ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya KGI Securities zinadai huwenda kampuni ya Apple ikazindua laptop mpya ya Macbook Air kabla ya nusu ya mwisho wa mwaka huu 2018.

Ripoti kutoka kwenye mtandao wa 9to5Mac, zinasema kuwa mwanaripoti huyo amesema Apple inategemea kuuza laptop hiyo mpya ya Macbook Air kwa bei nafuu zaidi chini ya Bei ya laptop hiyo kwa sasa ambayo inakadiriwa kuwa dollar $999 mpaka dollar $1200 ambayo ni sawa na shilingi za Tanzania Tsh 2,252,195.55 mpaka Tsh 2,705,340.00 (kwa mujibu wa viwango vya fedha vya siku ya leo).

Ni muda sasa umepita toka kampuni ya Apple kuzindua laptop mpya, lakini kwa mujibu wa mwanaripti huyo Apple inatarajiwa kuja na laptop mpya mwaka huu ikiwa pamoja na mfumo mpya wa uendeshaji wa iOS 11.3 na MacOS 11 mfumo unao tegemewa kuwa na maboresho mengi zaidi.

Advertisement

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use