in

Mabasi Mapya 70 ya Mwendokasi Yapokelewa Dar es Salaam

Mabasi haya mapya yanauwezo wa kuchukua abiria wengi zaidi

mabasi ya mwendokasi
Picha na AzamTV

Hivi karibuni, Kampuni ya mabasi yaendayo haraka (UDART) imepokea mabasi mapya 70 yenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 100 tofauti na magari ya awali yaliyoletwa katika awamu ya kwanza ya mradi wa huo

Taarifa kutoka kwenye mtandao wa Azamtv zinasema kuwa, mabasi hayo yamepokelewa katika Bandari ya Dar es Salaam ambapo inasemekana ujio wa mabasi hayo utaongeza ufanisi zaidi katika kutoa huduma pamoja na kuzalisha ajira mpya hapa jijini dar es salaam.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Katika upokeaji wa mabasi hayo siku chache zilizopita mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya (UDART), Charles Nawe amesema, tofauti ya ubora uliopo kati ya mabasi hayo mapya na ya awali ni muundo wa mabasi hayo pamoja na uwezo wa kuchukua abiria wengi kwa wakati mmoja.

Hata hivyo kwa mujibu wa mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya magari yaendayo haraka UDART Charles Nawe aliye ongea na Azamtv, alisema kuwa mabasi hayo yataendelea na safari za barabara zilizopo sasa hadi pale watakapo anzisha barabara nyingine zinazo tegemewa kuanzishwa miaka ya karibuni.

Mpaka sasa inasemekana Kampuni ya UDART ina jumla ya mabasi ya mwendokasi takribani 210 huku maitaji yakiwa ni takribani mabasi 305 kwa jijini dar es salaam.

Mabasi Mapya 70 ya Mwendokasi Yapokelewa Dar es Salaam
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.