in

Zifahamu Hizi Hapa Sifa za Simu Mpya ya Tecno Camon CM (2018)

Sasa simu hii inakuja na kioo bora cha Full Display pamoja na uwezo zaidi

Sifa za Tecno Camon CM 2018

Kampuni ya Tecno imerudi tena na simu yake mpya yenye muonekano bora simu ya Tecno Camon CM (2018), simu hii imekuja ikiwa simu ya kwanza kutoka kampuni ya Tecno yenye kioo cha kisasa cha aspect ration ya 18:9 Full Display pamoja na mfumo mpya wa uendeshaji. Simu hii pia inapatikana kwa bei nafuu na ina muonekano bora pengine kuliko simu nyingine za Tecno.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Sifa za Tecno Camon CM 2018

  • Aina ya Kioo  – Full Vision capacitive touchscreen
  • Ukubwa wa Kioo – 5.65-inch yenye resolution ya 720 x 1440 pixels
  • Uwezo wa SIM – Line mbili ndogo
  • Uwezo wa Network – 2G/3G/4G
  • Uzito wa Simu – 144g
  • Kamera ya Nyuma – Megapixel 13 yenye FF pamoja na Ring-Flash (Quad-Flash)
  • Kamera ya Mbele – Megapixel 13 yenye FF, pamoja na Dual-Flash
  • Uwezo wa Processor – Quad-Core 1.3GHz yenye uwezo wa 64-bit MEDIATEK MTK6737H
  • Uwezo wa GPU – Mali-T720
  • Ukubwa wa Ndani – GB 16 inayoweza kuongezeka kwa memory card hadi 128GB
  • Ukubwa wa RAM – GB2
  • Uwezo wa Sensors – inayo sensor za G-Sensor, Fingerprint, Ambient Light Sensor, Proximity Sensor and E-Compass
  • Mfumo wa uendeshaji – Android 7.0 Nougat yenye HiOS 2.0 User Interface
  • Uwezo wa Bluetooth – V4.1
  • Uwezo wa Battery – battery ya Li-Polymer yenye ukubwa wa 3050mAh, pamoja na teknolojia ya Fast Charging.
  • Mengineyo – Inayo fingerprint, inayo radio, kava lake ni la chuma.

Kwa sasa simu hii inapatikana kenya na inapatikana kwa shilingi za kenya Ksh 13000 sawa na shilingi za Tanzania Tsh 300,000, kumbuka bei inaweza kubadilika kwa Tanzania. Na hiyo ndio simu mpya ya Tecno Camon CM (2018), iliyo zinduliwa hivi karibuni. Kupata habari za simu hii endelea kutembea Tanzania Tech.

Soma HapaSimu 10 Bora za Tecno Mwaka 2018, Bei Zake Pamoja na Mahali Pakununua Simu Hizo.

Kwa habari zaidi za teknolojia hakikisha una download App yetu mpya ya Tanzania Tech kupitia Play Store na vilevile tembelea channel yetu ya Tanzania Tech kupitia Youtube ili uweze kujifunza zaidi mambo yote ya teknolojia kwa njia ya Video.

Zifahamu Hizi Hapa Sifa za Simu Mpya ya Tecno Camon CM (2018)
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Infinix na JBL Waungana Tena Na Sasa Ni Infinix Note 40

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa majibu kwa KetonGhairi kujibu

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

10 Comments