in

Naibu Mwenyekiti wa Samsung Kufungwa Miaka 12 Jela

Waendesha mashtaka wataka mkuu wa Samsung afungwe miaka 12

Samsung gEREZAN

Waendesha mashtaka nchini Korea Kusini wanataka naibu mwenyekiti wa kampuni ya Samsung Lee Jae-yong kupewa kifungo cha miaka 12 jela. Bwana Lee anakabiliwa na mashtaka kufuatia wajibu wake katika sakata la ufisadi, iliyosababisha rais wa zamani Park Gue-hye aondolewe madarakani. Imeripoti tovuti ya BBC.

Hata hivyo Inaripotiwa kuwa Lee alitoa pesa nyingi ili apate uungwaji mkono wa serikali kwaajili ya manufaa yake pekee, aidha inaripotiwa kuwa mwenyekiti huyo alikamatwa na amekuwa gerezani tangu mwezi Februari kufuatia sakata hilo.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kwa sasa bado mwenyekiti huyo anakana kufanya lolote baya, lakini katika hali nyingine siku ya mwisho ya kusikilizwa kwa kesi yake, waendesha mashtaka wa korea kusini walimtaja kuwa mtu aliye nufaika kutokana na uhalifu uliofanyika wakati wa sakati hilo na kutaka ahukumiwe.

Waendesha mashtaka wanamlaumu bwana Lee na wakurugenzi wengine wanne, kwa kumhonga mshirika wa karibu wa Rais Park, Bi Choi Soon-sil mamilioni ya dola ili wapate kupendelewa

Waendesha mashtaka walidai kuwa ufisadi huo ulikuwa na lengo la kupata uungwaji mkono wa serikali kwa mabadiliko ndani ya kampuni ya Samsung, Hukumu ya Lee inatarajiwa kutolewa tarehe 27 mwezi huu wakati akiendelea kusota gerezani.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya Video.

Chanzo : BBC 

Naibu Mwenyekiti wa Samsung Kufungwa Miaka 12 Jela
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.