Muigizaji The Rock Kuungana na Apple Kwaajili ya Filamu Mpya

Sasa jiandae na filamu mpya kutoka kampuni ya Apple
SIRI SIRI

Kama wewe ni mpenzi wa filamu pamoja na teknolojia kwa ujumla basi leo tuna habari hii njema kwaajili yako. Katika kutangaza bidhaa zake kampuni ya Apple imeingia mkataba na muigizaji maarufu nchini marekani maarufu kama Dwayne Johnson au kwa jina la uigizaji “The Rock”.

Mkataba huo ambao ni katika kutangaza programu ya SIRI ya kampuni hiyo muigizaji huyo anategemewa kutoa filamu yake mpya ambayo itakuwa ikitangaza bidhaa hiyo kutoka kampuni ya Apple. Filamu hiyo ambayo imepewa jina la The Rock X Siri inategemewa kutoka hivi karibuni na tayari apple wamekuwekea utangulizi huu.

https://www.youtube.com/watch?v=ufBLI6bB9sg

Advertisement

Lakini mpaka sasa bado haijajulikana filamu hiyo itatoka lini lakini kwa mujibu wa tweet iliyotumwa kwenye ukurasa wa muigizaji huyo, filamu hiyo inategemewa kutoka tarehe za karibuni na kwa muonekano wa picha ya tangazo filamu hiyo inategemewa kuwa ya Action na vichekesho vya hapa na pale.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.

Chanzo : The Next Web

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use