in

Mgahawa wa KFC Wazindua Simu ya Mkononi Huko Nchini China

Kusherekea miaka selathini ya huduma nchini china KFC yaja na hii

Simu janja ya KFC

Teknolojia inaendelea kukuwa sana, kiasi kwamba hata sehemu ambazo zilikua hazihitaji teknolojia basi sasa zimeanza kuweka teknolojia mbalimbali. Kuthibitisha maneno hayo hivi karibuni kampuni ya KFC imeadhimisha miaka 30 ya kutoa huduma za chakula huko nchini china na kuamua kuzindua smartphone yake.

Katika maadhimisho hayo kampuni hiyo ya KFC imeungana rasmi na kampuni maarufu ya kutengeneza simu ya Huawei ili kutengeneza simu hiyo janja ambayo itakuwa maalum kwa ajili ya kusindikiza kusherekea miaka 30 ya migahawa hiyo huko nchini china.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Simu hiyo ambayo inakuja na rangi nyekundu ikiwa na picha ya utambulisho ya KFC pamoja na mwaka ambapo migahawa hiyo ilifunguliwa kwa mara ya kwanza huko nchini China. Kuhusu sifa za Simu hiyo ya KFC inakuja na ukubwa wa ndani wa GB 32 huku ikiwa na programu nyingi zenye kuweza kurahisisha huduma za mgahawa huo nchini humo.

Baadhi ya programu hizo ni pamoja na programu ya kukusaidia kuagiza kuku mbalimbali kutoka kwenye mgahawa huo pamoja na programu ya kukusaidia kuchagua aina gani ya mziki unaotaka kusikia unapokua kwenye mgahawa huo. Hata hivyo bado kampuni ya KFC haija tangaza lini simu hiyo itangia sokoni na kwa bei gani lakini habari kutoka mitandao mbalimbali zinasema huenda simu hiyo ikaanza kuuzwa huko nchini china kupitia mtandao maarufu wa Alibaba.

KFC sasa imekua ni moja kati ya mghawa mkubwa sana duniani na hivi sasa unaonekana kuanza kutumia sana teknolojia kutoa huduma zake mara baada ya hivi karibuni kutangaza kuleta teknolojia ambayo itaweza kutambua chakula unachotaka kula kwa kuangalia hali sura yako.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.

Mgahawa wa KFC Wazindua Simu ya Mkononi Huko Nchini China
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Infinix na JBL Waungana Tena Na Sasa Ni Infinix Note 40

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.