Je Wajua: Hii Hapa Ndio Historia Fupi ya (#) Hashtag Ilipotoka

Kama ulikua bado hutambui hii hapa ndio historia fupi ya Hashtag
Hashtag Hashtag

Wote tunaijua au tumesha itumia hashtag #, lakini ni wachache sana kati yetu tunaejua historia ya hashtag ilipo tokea kifupi ni kwamba hashtag imeanzia bali sana na kama wewe ni mmoja wa watu ambao wanataka kujua historia ya hashtag # basi ifuatayo ndio historia yake fupi.

Manamo mwaka 2007 mwezi August Chris Messina, mtaalamu wa mitandao ya kijamii aligundua hashtag ya kwanza ambayo ilikua ikitumika kwenye mtandao wa Twitter, hashtag hiyo ilikua maalum kwaajili ya kukusanya maongezi yote ambayo yalikua yakihusu kampuni iliyokuwa inaitwa Barcamp hashtag hiyo ilikua ni #barcamp.

Tukirudi nyuma kidogo hashtag ilikua ikitumika kwenye IRC au Internet Relay Chat mfumo wa zamani wa kuchati ulio kuwa ukitumiwa na makampuni mbalimbali. Kuhusu jina Hashtag lilipotoka bado historia nzima ya neno hilo haijawekwa wazi bali kwa mujibu wa tovuti mbali mbali mtandaoni neno hilo limetokana na neno “tag” na limegunduliwa na wagunduzi wa mtandao wa Twitter.

Advertisement

Na hiyo ndio historia fupi ya hashtag ilipotokea, bado historia hii haiakamilika kutokana na kuwa na makala mbalimbali zenye kusema tofauti uhalisia wa neno hilo ila ni uhakika hashtag ya kwanza ilianza kutumika hapo mwaka 2007 na ilitumiwa na Chris Messina kwenye mtandao wa Twitter na hiyo hapo chini ndio Tweet yenyewe.

https://twitter.com/chrismessina/status/223115412

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use