Uber Yasimamisha Majaribio ya Magari Yanayo Jiendesha

Uber imechukua uamuzi huo baada ya ajali iliyotokea huko Arizona
Uber Uber
PICHA NA REUTERS

Kampuni maarufu ya usafirishaji ya Uber hivi karibuni imekubwa na masaibu mengine baada ya kusitisha majaribio ya magari yake yanayo jiendesha, masaibu hayo yameikumba kampuni hiyo baada ya moja ya magari yake yanayo jiendesha kupata ajali huko Arizona nchini marekani.

Ajali hiyo ilitokea kwenye barabara ya Arizona roadway ambapo gari hilo lilipata ajali na kupinduka uku likiacha magari mengine mawili yakiwa yameumia kwa upande wa Ubavuni. Habari zilizotolewa na tovuti ya tech2 zinasema kuwa, kampuni hiyo imeamua kusimamisha majaribio ya magari hayo huku ikipisha mapolisi wa usalama wa barabarani kufanya uchunguzi ili kujua kilicho tokea.

Kwa bahati nzuri ajali hiyo haiku sababisha mtu yoyote kupoteza maisha lakini hii sio mara ya kwanza kwa magari yanayo jiendesha kupata ajali, mwaka 2016 mwendeshaji wa magari yanayo jiendesha ya Tesla aliuwawa baada ya gari linalo jiendesha kutoka kampuni ya Tesla Motors Inc kupata ajali kwa kugongana na Roli huko Williston, Florida nchini marekani, Vilevile kampuni ya Google nayo ilisha tokea kwenye vichwa vya habari kutokana na magari yake yanayo jiendesha kuhusushwa na Ajali mbalimbali za barabarani.

Advertisement

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia unaweza kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja ya teknolojia kwa video.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use