in

Sifa za Simu Mpya za Huawei Nova na Huawei Nova Plus

Mwanzoni mwa mwezi September Huawei ilizindua simu zake mpya za Huawei Nova na Nova Plus, Hizi ndio sifa za simu hizo

Huawei Nova

Mwanzoni mwa mwezi September Huawei ilitoa simu zake mbili mpya ambazo zilikuja na majina mapya kabisa kutoka kwenye kampuni hiyo maarufu ya china, simu hizo ambazo ni Huawei Nova pamoja na Huawei Nova Plus zilizinduliwa kwenye mkutano wa IFA uliofanyika hvi karibuni.

Japo kuwa pengine simu za Huawei Nova na Huawei Nova Plus zinaonekana kama ziko sawa ila simu hizi ni tofauti kwa namna yake ukiacha swala la kufanana kwa majina pamoja na muundao wa simu hizo. Basi kama umefikiria kununua simu hizi, sifa hizi zifuatazo zitakusaidia wewe kuweza kufanya uamuzi mrahisi kuhusu ni simu gani ya kununua kati ya Huawei Nova au Huawei Nova Plus.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

SIFA ZA HUAWEI NOVA

  • Inayo uwezo wa Network wa GSM / HSPA pamoja na LTE (4G)
  • Kava la nje lina ukubwa wa 141.2 x 69.1 x 7.1 mm (5.56 x 2.72 x 0.28 in)
  • Uzito wa simu ni 146 g (5.15 oz)
  • Inatumia Line Mbili ambazo ni za Kukata au (Nano-SIM) or Dual SIM
  • Inayo Wireless yenye nguvu ya 802.11 b/g/n, pamoja na teknolojia za Wi-Fi Direct na hotspot
  • Teknolojia ya Bluetooth Toleo la 4.1, A2DP, LE
  • Teknolojia ya Kioo inatumia IPS LCD capacitive touchscreen, 16M colors
  • Ukubwa wa Kioo ni 5.0 inches (~70.6% kuanzaia kwenye kioo mpka kwenye kava)
  • Uwezo wa Kioo ni 1080 x 1920 pixels (~441 ppi pixel density)
  • Unaweza Kukusa Kioo kwa Vidole viwili yani Multitouch
  • Teknolojia ya Mfumo wa Uendeshaji ni Emotion 4.1 UI kutoka Huawei
  • Mfumo wa Uendeshaji ni Android ambayo ni toleo la 6.0.1 (Marshmallow)
  • Processor ni Chipset Qualcomm MSM8953 Snapdragon 625
  • Nguvu ya Processor ni Octa-core 2.0 GHz Cortex-A53 GPU Adreno 506
  • Inayo uwezo wa kuweka memory kadi ya ukubwa mpaka GB 256
  • Memory ya Ndani ya Simu ni 32GB Pamoja na RAM ya GB 3
  • Kamera ya Nyuma ni MP 12, yenye teknolojia za phase detection autofocus, LED flash, yenye uwezo wa kuchuka Video za 2160p kwa 30fps
  • Kamera ya Mbele ni MP 8
  • Kuhusu Radio Bado Hakuna uhakika
  • Battery isiyo yakutoa yenye uwezo wa mAh 3020 iliyo tengenezwa kwa teknolojia ya  Li-Po
  • Inatumia Chaji yenye kiunganishi cha Type-C 1.0
  • Inapatika kwa rangi za Prestige Gold, Mystic Silver, Titanium Grey
  • Bei iliyotangazwa ni kwa nchi za Europe ambayo ni 399£ euros ambayo ni sawa na Shiling za kitanzania Tsh 971,374.59 kwa mujibu wa viwango vya kubadilisha fedha vya leo tarehe 30-09-2016

SIFA ZA HUAWEI NOVA PLUS

  • Inayo uwezo wa Network wa GSM / HSPA pamoja na LTE (4G)
  • Kava la nje lina ukubwa wa 151.8 x 75.7 x 7.3 mm (5.98 x 2.98 x 0.29 in)
  • Uzito wa simu ni 160 g (5.64 oz)
  • Inatumia Line Mbili ambazo ni za Kukata au (Nano-SIM) or Dual SIM
  • Inayo Wireless yenye nguvu ya 802.11 b/g/n, pamoja na teknolojia za Wi-Fi Direct na hotspot
  • Teknolojia ya Bluetooth Toleo la 4.1, A2DP, LE
  • Teknolojia ya Kioo inatumia IPS LCD capacitive touchscreen, 16M colors
  • Ukubwa wa Kioo ni 5.5 inches (~72.6% kuanzaia kwenye kioo mpaka kwenye kava)
  • Uwezo wa Kioo ni 1080 x 1920 pixels (~401 ppi pixel density)
  • Unaweza Kukusa Kioo kwa Vidole viwili yani Multitouch
  • Teknolojia ya Mfumo wa Uendeshaji ni Emotion 4.1 UI kutoka Huawei
  • Mfumo wa Uendeshaji ni Android ambayo ni toleo la 6.0.1 (Marshmallow)
  • Processor ni Chipset Qualcomm MSM8953 Snapdragon 625
  • Nguvu ya Processor ni Octa-core 2.0 GHz Cortex-A53 GPU Adreno 506
  • Inayo uwezo wa kuweka memory kadi ya ukubwa mpaka GB 256
  • Memory ya Ndani ya Simu ni 32GB Pamoja na RAM ya GB 3
  • Kamera ya Nyuma ni MP 16, yenye teknolojia za phase detection autofocus, LED flash, yenye uwezo wa kuchuka Video za 2160p kwa 30fps
  • Kamera ya Mbele ni MP 8
  • Inayo FM Radio
  • Battery isiyo yakutoa yenye uwezo wa mAh 3340 iliyo tengenezwa kwa teknolojia ya  Li-Po
  • Inatumia Chaji yenye kiunganishi cha Type-C 1.0
  • Inapatika kwa rangi za Prestige Gold, Mystic Silver, Titanium Grey
  • Bei iliyotangazwa ni kwa nchi za Europe ambayo ni 429£ euros ambayo ni sawa na Shiling za kitanzania Tsh 1,044,410.27 kwa mujibu wa viwango vya kubadilisha fedha vya leo tarehe 30-09-2016

Na hizo ndio sifa za Simu mpya za Huawei Nova pamoja na Huawei Nova Plus ili kujua zaidi kuhusu simu hizi lini zitafika Tanzania endelea kutembelea blog ya Tanzania tech kila siku au unaweza kupata habari zote za teknolojia moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi kwa ku-download App ya Tanzania tech  kwenye simu yako ya Android, au pia unaweza kujiunga nasi kwa barua pepe pamoja na mitandao yetu ya kijamii ya Facebook, Twitter, Instagram pamoja na Yotube  ili kupata habari mbalimbali za teknolojia pamoja na kujifunza mambo ya teknolojia kwa njia ya video.

Sifa za Simu Mpya za Huawei Nova na Huawei Nova Plus
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Zifahamu Hizi Hapa Bei za Simu Mpya za Redmi Note 13

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.