Chaji ya Simu Yenye Kuchaji Simu yako Uku Ikielea

Chaji simu yako kwa kutumia wireless chaji hii yenye kuchaji simu kwa kutumia teknolojia mpya
chaji ya simu chaji ya simu

Teknolojia imendelea ku-kua sana hizi siku za usoni, hivi karibuni uko marekani wana teknolojia kutoka katika kampuni ya AR Designs wamefanikiwa kutengeneza chaji isiyotumia waya yenye uwezo wa kuchaji simu yako uku ikielea hewani.

https://www.youtube.com/watch?v=jKOEndleQFc

Chaji hiyo iliyotengenezwa hivi karibuni imetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya induction pamoja na Electromagnetism, teknolojia hizi zimeunganishwa ili kukamilisha kifaa hichi ambacho kitachaji simu yako kwa njia bora na ya kisasa kabisa hata hivyo, akielezea jinsi kifaa hicho kinavyofanya kazi kiongozi wa kampuni ya AR Designs Rukhsana Perveen alisema ” teknolojia hizi mbili zimeunganishwa kwa pamoja ili kusaidiana kuleta chaji ambayo ningependa kuiita kama chaji ya kizazi kipya, teknolojia ya induction ndio inayo usika na kuanya kifaa hicho kuchaji simu yako wakati teknolojia ya electromagnetism ndio inayosababisha simu yako kuelea pale unapoichaji ” alisema kiongozi huyo.

Advertisement

Chaji hiyo inategemewa kuuzwa kwa dollar za kimarekani $229 ambayo ni sawa na shilingi za kitanzania TSH 500960.40 hata hivyo upatikanaji wa chaji hizo utaanza rasmi mwezi December mwishoni mwa mwaka huu.

Kwa kupata habari zaidi unaweza kuungana nasi kupitia barua pepe (email) na tutakujulisha pindi tu habari mpya itakapo ingia kwenye tovuti yetu ya Tanzania tech, pia unaweza kutufuata kwenye mitandao ya kijamii ya  facebook, Instagram, Twitter na Youtube Channel ili kupata video za habari na mafunzo ya teknolojia mbalimbal

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use