Sasa Unaweza Ku-qoute Meseji Kwenye Whatsapp

whatsapp qoute whatsapp qoute

Programu bora ya kuchat ya Whatsapp sasa inauwezo wa ku-qoute meseji pale unapokua unachati, sehemu hii mpya ya programu hiyo inasaidia sana hasa kwa wale wanao chati kwenye ma-group mbalimbali kwa mfano inawezekana labda ujasoma meseji zako za whatsapp kwa muda mrefu na imetokea umekuta meseji zaidi ya 100 labda meseji moja au mbili zinakuitaji kujibu hapo inakuwa tatizo kidogo tena ikitegemewa kuwa tayari watu walisha endelea kuzungumzia mambo mengine kwenye group hilo.

Lakini kwa kutumia sehemu hii mpya unakua na uwezo wa kujibu meseji ya mtu hata kama ilikupita muda mrefu, ili kujua kama sehemu hiyo imewezeshwa kwenye simu yako ingia kwenye programu yako ya whatsapp kisha kwenye meseji unayotaka kujibu au ku-qoute kisha bofya na ushikilie kwa sekunde moja kisha utaona mshale wenye alama kama unaelekea upande wa kushoto bofya hapo na utaona meseji ya mtu unayetaka ku-qoute ikipanda juu na hapo itakupa uwezo wa kujibu meseji ya mtu huyo ikiwamo na meseji uliyoandikiwa hapo awali.

Kama bado huja pata sehemu hii muhimu unaweza ku-uninstall au kufuta programu  hiyo ya whatsapp na ku-install tena upya kisha kama bado hujaiona sehemu hiyo subiri kwa siku kadhaa kisha ujaribu tena.

Advertisement

Kama umeipenda hii usisite kulike page yetu ya Facebook pamoja na Twitter ili kupata habari mpya pindi zinapotoka, pia kwa kujifunza mambo mbalimbali kwa vitendo unaweza ku subscribe kwenye Youtube Channel yetu hapa Tanzania tech blog.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use