Jinsi ya Kurudisha Picha Zilizofutika Kwenye Simu Yako ya Android

Jinsi ya Kurudisha Picha Zilizofutika Kwenye Simu Yako ya Android Jinsi ya Kurudisha Picha Zilizofutika Kwenye Simu Yako ya Android

Kuna wakati inatokea unafuta picha zako kwenye simu yako kwa bahati mbaya au hata kuna muda tu unataka kurudisha picha zako ulizowahi kuzifuta kutoka kwenye simu yako kama unataka kufanya hayo yote basi usijali kwani leo tutaenda kujifunza namna rahisi ya kurudisha picha zako hizo kwenye simu yako kwa namna rahisi kabisa.

Hata hivyo kama inavyojulikana watu wengi sana wanajua namna ya kurudisha picha zilizopotea kwenye kompyuta lakini watu wengi hawajui kufanya hivyo ikija katika swala zima la Smartphone au (Android Phones) au hata simu nyingine za mkononi, hivyo basi leo tutajifunza hatua kwa hatua namna ya kufanya hivyo bila kutumia muda mwingi.

Advertisement

Kwa kuanza basi ili kuweza kufanikisha hili unahitaji kuwa na bando atlist MB100 kwaajili ya kupakua programu kutoka kwenye PlayStore kingine unatakiwa kuhakikisha kuwa simu yako iko ROOTED (Bofya hapa kuangalia namna ya ku-root simu yako) ukisha fuata maelezo hayo na kuhakikisha simu yako iko rooted endelea kipengele cha pili ambapo ni kupakua Programu ya Android iitwayo (DiskDigger) bofya hapo chini kupakua programu hiyo ya android kwenye simu yako.

Baada ya hapo install programu hiyo kisha ruhusu programu hiyo kupitia superuser  baada ya hapo chagua file lenye picha zilizo potea alafu chagua format kama ni jpg, png au hata mp4 kisha acha programu hiyo ifanye scaning baada ya hapo moja kwa moja utaweza kurestore picha zako na hata video.

Kama umeipenda hii usisite kulike page yetu ya Facebook pamoja na Twitter ili kupata habari mpya pindi zinapotoka, pia kwa kujifunza mambo mbalimbali kwa vitendo unaweza ku subscribe kwenye Youtube Channel yetu hapa Tanzania tech blog. Pia usisahau kubofya hako ka-LOVE hapo chini ili ku-show love..!!

32 comments
  1. mimi nimefuta picha zangu lakini kila nkidownload hazikubali kwa nini naomba mnisaidie au nipigieni kwenye namba hii 0776333022 au 0719882437 niwafuate popote mulipo na ntalipa gharama zote kwenye wasap ukisevu namba hii utaniona au fb email yangu ni [email protected] nipo unguja mtu yoyote atakae uona ujumbe huu naomba anisaidie

          1. Nikijaribu kufungua faili langu LA Instagram inaniomba password na sikuweka password nifanyeje

  2. Nashukuru sana kwa hilo . Ila nilitaka kufahamu jinsi Gani ya kuwezesha Simu Yangu kurudisha nyimbo pia , na mambo mengine?

    1. Hapana hiyo app inahifadhi picha kwenye simu yako hivyo simu yako ikipotea basi na picha zimepotea. Sorry

  3. Msaada,jinsi rejesha picha ambazo zimefutika na ukiwa umefunguwa akaunti nyingine unafanyaje mbaya zaidi nimesahau namba ya siri

    1. Ni ngumu sana kupata picha kutoka kwenye akaunti ambayo umesahau password, muhimu ni kuhakikisha unafanyia kazi swala la kupata password alafu swala la kurudisha picha litafuata.

  4. Jaman mimi sijafuta Picha ila tu Picha zoote upande wa camera zimepotea na hii ni Mara ya pili Sasa Sasa sijui tatizo ni sim au nazifuta bila kujua natumia sim aina ya Camon X nisaidien tafadhali

  5. Anaitwa Rosemary Tikiti.nimefuta picha za harusi ya mwanangu kwa bahati mbaya nisaidie nizipate tena kila nikisoma maelekezo sielewi.

Toa majibu kwa Ttech Geek Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use