Huduma za Taxi za Uber Zaja Jijini Dar es Salaam

uber kuja dar es salaam uber kuja dar es salaam

Kampuni inayotoa huduma za usafirishaji ya nchini marekani ijulikanayo kama UBER inategemewa kuja jijini dar es salaam siku za usoni, kampuni hiyo ambayo imejikita katika swala la usafirishaji inatumia teknolojia ya kisasa ili kuwezesha mteja kupata usafiri mahali popote pale alipo na kwa urahisi kabisa.

Uber imeanza kufanya matangazo yake kupitia mtandao wa facebook ambapo kampuni hiyo kwa sasa inahitaji watu wenye magari na ambao wengependa kuanza biashara ya usafirishaji ya kisasa kabisa hata hivyo kampuni hii inategemewa kuingia kwenye miji ya Accra uko Ghana, Dar es Salaam Tanzania na Kampala uko Uganda.

Akiujiwa na vyombo vya habari mwezi march mwaka huu maneja wa kampuni hiyo kwa africa alisema ” kampuni ya uber inategemea kujipanua kwa nchi nyingi africa kutokana na kwamba watu wengi mbalimbali wameonekana wakitafuta usafiri wa haraka na ambao unaweza kutegemewa kwa wakati wowote” hata hivyo ndani ya mwezi huo wa tatu kampuni hiyo ilifungua matawi yake pamoja na huduma zake kwenye miji ya afrika ya Abuja uko Nigeria na Mombasa uko Kenya.

Advertisement

Uber - Request a ride

Kampuni hiyo ya Uber ilifungua website yake mpya ambayo kwa sasa kampuni hiyo inatafuta madereva pamoja na Operations Coordinators, kama unavigezo unaweza kubofya hapa na ku-apply kazi hiyo kutoka uber Apply HapaPia kama unalo gari na ungependa kujisajili kuwa dereva na kujipatia kipato freshi na kiurahi jiunge kwa ku-Bofya Hapa.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use