in

Smartphone Aina ya Zuri Zaja Africa Mashariki

Smartphone Aina ya Zuri Zaja Africa Mashariki

Kampuni inayotengeneza simu za aina ya ZURI ambayo ina makao makuu yake huko Hong Kong imetangaza kuanza kusambaza bidhaa zake kwa nchi za Afrika Mashariki yani Kenya, Tanzania na Uganda, kampuni hiyo ilitangaza kuungana na kampuni iitwayo Despec ili kufanikisha zoezi hilo la kusambaza simu hizo kwa nchi za afrika mashariki.

Kiongozi wa kampuni hiyo alisema simu ambazo zitakuja kwenye nchi za afrika mashariki ni pamoja na Zuri C41, C46, C52 pamoja na S56. Mwenyekiti huyo Vikash Shah, aliendelea kusema ” nchi za afrika mashariki zinatoa uwezo zaidi wa kukua kwa simu ya ZURI kutoka na kuongezeka kwa mahitaji ya simu za mkononi pia tunaamini kuwa DESPEC ndio mshirika wetu mzuri atakae tusaidia kukua kupitia nchi hizo za afrika mashariki”.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Tukiangalia katika simu hizo za ZURI zinasifa ya kioo cha inch 4.0 kwa simu zake zote ikiwa na RAM ya 512MB mpaka RAM 1GB kwa Zuri C41 hadi S56 pia simu hiyo inauwezo wa Processor ya 1.3 GHz Quad-core hadi processor ya 1.4 GHz Octa-core processo kwa simu zake hizo.

Pia kiongozi wa kampuni ya DESPEC alisema kuwa “tunafurahi kuwa na kampuni ya ZURI kama sehemu ya kampuni yetu, kwani jina la kampuni hii linafanana na ubora wa bidhaa hizo hivyo kampuni hiyo inaonyesha kabisa ya kuwa itapata matokeo mazuri afrika mashariki kutokana na ubora wake” alisema Riyaz Jamal kiongozi wa kampuni hiyo ya DESPEC.

 

Smartphone Aina ya Zuri Zaja Africa Mashariki
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Zifahamu Hizi Hapa Bei za Simu Mpya za Redmi Note 13

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.