in

Jinsi ya Kuongeza Like na Follower Kwenye Instagram na Facebook

Facebook Like

Kama wewe ni mfanya biashara nadhani utakubaliana na mimi kuwa kuanza biashara pekee ni zoezi kubwa sana linaloitaji muda pamoja na pesa, vilevile inapokuja katika swala la kutafuta masoko kwaajili ya biashara yako bado inakua ni mthihani hii inatokana na upya wa biashara yako lakini shukurani kwa mitandao ya kijamii siku hizi unaweza ukawa na akaunti za mitandao ya kijamii na moja kwa moja ukaanza kupata wateja kwenye biashara yako mpya.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Bila shaka kila mtu yuko kwenye mitandao ya kijamii lakini sio watu wote wenye like na follower wa kutosha kwenye mitandao hiyo kuna baadhi ya watu wako kwenye mitandao ya kijamii kwa miaka sasa lakini bado hawana like au follower wakutosha. Je unafanyaje kuongeza hawa follower na like ili uweze kuanza kutafuta masoko kwaajili ya biashara yako ? jibu lipo hapa hapa kwenye ukurasa huu, hivyo basi bila kupoteza muda moja kwa moja twende tukaanze somo letu.

Kwanza kabisa ingia katika akaunti yako ya Facebook na copy link iliopo kwenye kisanduku cha link kilichoko juu kwenye browser yako kama inavyoonekana kwenye picha.

screenshot_20160408_083846 (2)

Alafu ingia kwenye tovuti hii [button type=”default” text=”http://bit.ly/1Mi3HN1″ url=”http://bit.ly/1Mi3HN1″ open_new_tab=”true”] kisha chagua register kisha ujaze kila kitu sahihi kama inavyotakiwa kwenye fomu hiyo iliyoko kwenye tovuti hiyo.

screenshot_20160408_093719 (1)

Subiri kidogo kisha hakiki akaunti yako kwa kuingia kwenye email yako na ingiza namba za siri ambazo zitakua kwenye email ambayo itakua na kichwa cha habari “Like4Like.org e-mail verification”

screenshot_20160408_095644

Weka namba hizo kisha utaletwa kwenye sehemu ambayo utaona umepewa credit au pointi 30 ambapo sasa unaweza kuweka akaunti zako tayari kwa kuanza kuongeza followers na likes kwenye kurasa zako za facebook na instagram.

screenshot_20160408_100242 (1)

Bofya kwenye sehumu ilioandikwa “add and manage page”  kisha uanze kuweka kurasa zako kama inavyoonyesha kwenye picha hapo chini.

screenshot_20160408_101025

Kisha chagua option ya kwanza ambayo imeandikwa “Facebook Likes” ambayo iko upande kwa kushoto juu kabisa kama inavyoonyesha kwenye picha hapo chini.

screenshot_20160408_101615

Rudi kwenye akauti yako ya facebook copy link yako kisha iweke kwenye sehemu iliyo andikwa “Facebook URL” kisha andika ukurasa wako unahusu nini kwenye sehemu iliyoandikwa “Link Description” kisha chagua kiasi cha pointi ambazo ungependa mtu apate pale anapo like page yako chagua kwenye sehemu iliyoandikwa “Credits”.

screenshot_20160408_102351

Kisha bofya mahali palipo andikwa Add URL hapo utakua umesha weka akauti yako tumia hatua hiyohiyo kuweka akaunti yako ya instagram katika page hiyo. Baada ya hapo bogya mahali palipo andikwa “Social media Exchange”.

screenshot_20160408_103308

Kisha anza kwanza kwa kuangalia video za youtube kwani ndio njia rahisi ambayo itakusaidia kupata credit ambazo zitakusaidia wewe kupata like pamoja na followers kwenye page zako, pia unaweza ukachagua njia nyingine nyingi zilizopo ambazo pia zipo ambazo unaweza ku-like page ya mtu ili upate point endelea kuafanya hivyo na utaona point zikiongezeka ukiona zimepungua ujue kuwa kuna mtu tayari au watu wameanza kulike au kufollow page zako angalia akaunti zako huku ukiendelea kutafuta point zaidi na zaidi kwani kadri unavyopata point ndivyo unavyopata follower wengi zaidi.

Jinsi ya kuangalia video bofya kwenye sehemu yenye video ya youtube kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini.

screenshot_20160408_104400

Kisha bofya kitufe cha rangi ya blue kama picha inavyoonyesha kwenye picha hapo chini.

screenshot_20160408_104153

 

kisha video itatoke a hakikisha hautoki kwenye page hiyo angalia video kwa seconde chache kisha secunde zikiisha utaona imeandika “You have earned 14 credits!” hapo funga video hiyo na uendelee kuangalia zingine mpaka zote ziishe endelea hvyo kujiongezea pointi zaidi na jitahidi kila siku ufikishe kiasi flani cha crediti ili kujiongeze follower wengi zaidi.

screenshot_20160408_104122 (1)

Kwa msaada zaidi na namna ya kujifunza zaidi angalia video hiyo hapo juu na unaweza ku-comment ili kuelekezwa zaidi.

 

 

Jinsi ya Kuongeza Like na Follower Kwenye Instagram na Facebook
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Jinsi ya Kufuta Kwa Haraka Picha na Mafaili Yanayofanana

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

18 Comments