Hii Ndio Simu Mpya ya LG G5

Simu mpya za LG G5 Zazinduliwa hivi karibuni soma hapa habari kamili
Hii Ndio Simu Mpya ya LG G5 Hii Ndio Simu Mpya ya LG G5

Kama wewe ni mpenzi wa simu za LG hii inakuhusu sana, Kampuni kubwa ya electronic ya LG imetangaza kuzingua simu yake mpya ya LG G5. Taarifa kutoka katika blog ya habari za technolojia ya “Techradar” imetoa taarifa hizo kuwa LG watafanya uzinduzi huo wa simu yao hio siku ya tarehe 21 ya mwezi wa pili huko Barcelona ambako pia kunafanyka uzinduzi wa simu mpya ya “Samsung Galaxy S7”. Hata hivyo taarifa kutoka kwenye blog hiyo zinasema simu hiyo ya LG itakua na umbo la aluminum kwa nje ambalo litasaidia kulinda simu hiyoisipatwe na itlafu yoyote pale inapokutana na kitu cha chuma inapokua mfukoni au kwenye mikoba ya kinadada.

Taarifa zinaendelea kusema kua simu hiyo itakuja na mtindo mpya wa kutoa battery kama inavyoonekana kwenye mchoro hapo chini kutoka website maarufu ya Technology ya CNET ya korea.

Advertisement

Habari zinaendelea kusema kwamba simu hiyo ya LG G2 itakuja na Kamera yenye uwezo wa Mega Pixel 21, pia itakua na kava kama lile lililoonekana kwenye simu za samsung yani “Flip kava” kama inavyoonekana kwenye video hapo juu.

Kufuatilia habari za teknolojia kila siku endelea kutembelea blog ya tanzania tech kila siku au unaweza kupata habari zote za teknolojia moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi kwa ku-download App ya Tanzania tech  moja kwa moja kwenye simu yako ya Android, pia unaweza kujiunga nasi kwa barua pepe pamoja na mitandao yetu ya kijamii ya Facebook, Twitter, Instagram pamoja na Yotube kwa kujifunza mambo mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.

 

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use